Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 4:1-12 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Wana wa Yuda walikuwa Peresi, Hesroni, Karmi, Huri na Shobali.

2. Reaya, mwana wa Shobali, alimzaa Yahathi, aliyekuwa baba yake Ahumai na Lahadi, hizo ndizo jamaa za Wasorathi.

3. Wana wa Etamu walikuwa Yezreeli, Ishma na Idbashi. Walikuwa na dada mmoja aliyeitwa Haselelponi.

4. Penueli aliwazaa Gedori na Ezeri, na Ezeri akamzaa Husha. Hao ndio wazawa wa Huri mzaliwa wa kwanza wa Efratha, baba yake Bethlehemu.

5. Ashuru, mwanzilishi wa mji wa Tekoa, alikuwa na wake wawili: Hela na Naara.

6. Naara alimzalia wana wanne: Ahuzamu, Heferi, Temeni na Haahashtari.

7. Hela alimzalia wana watatu: Serethi, Ishari na Ethnani.

8. Hakosi aliwazaa Anubi na Sobeba, na ndiye aliyekuwa baba wa jamaa za wazawa wa Aharheli, mwana wa Harumu.

9. Kulikuwa na mtu mmoja jina lake Yabesi, aliyeheshimiwa kuliko ndugu zake wote. Mama yake alimpa jina la Yabesi kwa sababu alimzaa kwa maumivu.

10. Lakini Yabesi alimwomba Mungu wa Israeli akisema, “Ee Mungu, nakusihi unibariki na kuipanua mipaka yangu. Mkono wako uwe pamoja nami na unilinde kutokana na jambo lolote ovu, lisiniumize.” Naye Mungu akamjalia yale aliyoomba.

11. Kelubu, nduguye Shuha, alimzaa Mehiri na Mehiri akamzaa Eshtoni.

12. Eshtoni alikuwa na wana watatu: Beth-rafa, Pasea na Tehina. Tehina alikuwa mwanzilishi wa mji wa Ir-nahashi. Wazawa wa watu hawa waliishi Reka.

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 4