Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 27:29-32 Biblia Habari Njema (BHN)

29. Aliyesimamia mifugo iliyokuwa Sharoni alikuwa Shitrai, Msharoni; aliyesimamia mifugo iliyokuwa mabondeni alikuwa Shafati mwana wa Adlai.

30. Aliyesimamia ngamia alikuwa Obili Mwishmaeli. Aliyesimamia punda alikuwa Yedeya, Mmeronothi. Aliyesimamia makundi ya kondoo alikuwa Yazizi, Mhagri.

31. Hao wote walikuwa watunzaji wa mali ya mfalme Daudi.

32. Yonathani, mjomba wa mfalme Daudi, alikuwa mshauri na mtu mwenye ufahamu na mwandishi. Yeye na Yehieli mwana wa Hakmoni waliwafunza wana wa mfalme.

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 27