Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 23:5-23 Biblia Habari Njema (BHN)

5. 4,000 wawe mabawabu, na 4,000 wawe waimbaji, wakimsifu Mwenyezi-Mungu kwa ala za muziki alizotengeneza mfalme mwenyewe kwa madhumuni hayo.

6. Daudi aliwagawanya Walawi katika makundi matatu kulingana na koo za kabila la Lawi: Ukoo wa Gershoni, ukoo wa Kohathi na ukoo wa Merari.

7. Wana wa Gershoni walikuwa wawili: Ladani na Shimei.

8. Ladani alikuwa na wana watatu: Yehieli mkuu wao, Zethamu na Yoeli.

9. Wana wa Shimei walikuwa watatu: Shelomithi, Hazieli na Harani. Hawa walikuwa viongozi wa ukoo wa Ladani.

10. Wana wa Shimei walikuwa viongozi wanne: Yahathi, Zina, Yeushi na Beria.

11. Yahathi ndiye aliyekuwa mkuu wao, akifuatiwa na Ziza. Lakini Yeushi na Beria, kwa vile hawakuwa na wana wengi, walichukuliwa na ukoo mmoja.

12. Wana wa Kohathi walikuwa wanne: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.

13. Wana wa Amramu walikuwa Aroni na Mose. Aroni aliteuliwa awe akiweka wakfu vyombo vitakatifu kabisa, pia wazawa wake daima wafukizie ubani mbele za Mwenyezi-Mungu, wakimtumikia na kuwabariki watu katika jina la Mwenyezi-Mungu milele.

14. Lakini wana wa Mose, mtu wa Mungu, hutajwa miongoni mwa kabila la Lawi.

15. Wana wa Mose walikuwa Gershomu na Eliezeri.

16. Aliyekuwa mkuu miongoni mwa wana wa Gershomu ni Shebueli.

17. Eliezeri alikuwa na mwana mmoja tu; Rehabia, naye alikuwa kiongozi. Lakini Rehabia alikuwa na wana wengi sana.

18. Ishari alimzaa Shelomithi, kiongozi wa kabila zima.

19. Wana wa Hebroni walikuwa wanne: Mkuu wao alikuwa Yeria, wa pili Amaria, wa tatu Yahazieli na wa nne Yekameamu.

20. Wana wa Uzieli walikuwa wawili: Mika mkuu wao, na Ishia wa pili.

21. Merari alikuwa na wana wawili: Mali na Mushi. Wana wa Mali walikuwa wawili: Eleazari na Kishi.

22. Eleazari alifariki bila kupata mtoto wa kiume, ila mabinti tu. Mabinti hao waliolewa na binamu zao, wana wa Kishi.

23. Wana wa Mushi walikuwa watatu: Mali, Ederi na Yeremothi.

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 23