Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29

Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 1 Biblia Habari Njema (BHN)

Toka Adamu hadi Abrahamu

1. Adamu alimzaa Sethi, Sethi akamzaa Enoshi, Enoshi akamzaa Kenani,

2. Kenani akamzaa Mahalaleli, Mahalaleli akamzaa Yaredi,

3. Yaredi akamzaa Henoki, Henoki akamzaa Methusela. Methusela alimzaa Lameki,

4. Lameki akamzaa Noa. Noa alikuwa na wana watatu: Shemu, Hamu na Yafethi.

5. Wana wa Yafethi walikuwa Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi.

6. Wana wa Gomeri walikuwa Ashkenazi, Difathi na Togama.

7. Wana wa Yavani walikuwa Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu.

8. Wana wa Hamu walikuwa Kushi, Misri, Puti na Kanaani.

9. Wana wa Kushi walikuwa Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa Sheba na Dedani.

10. Kushi alimzaa Nimrodi, aliyekuwa mtu shujaa wa kwanza duniani.

11. Wazawa wa Misri ni Waludi, Waanamu, Walehabi, Wanaftuhi,

12. Wapathrusi Wakaftori na Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti).

13. Wana wa Kanaani walikuwa Sidoni, mzaliwa wake wa kwanza, na Hethi.

14. Kanaani pia ndiye babu yao Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,

15. Wahivi, Waarki, Wasini,

16. Waarvadi, Wasemari na Wahamathi.

17. Wana wa Shemu walikuwa Elamu, Ashuri, Arpaksadi, Ludi, Aramu, Usi, Huli, Getheri na Mesheki.

18. Arpaksadi alimzaa Shela, Shela akamzaa Eberi.

19. Eberi alikuwa na wana wawili; mmoja wao aliitwa Pelegi, (kwa maana wakati wake watu walikuwa wametawanyika duniani), na ndugu yake aliitwa Yoktani.

20. Wana wa Yoktani walikuwa Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,

21. Hadoramu, Uzali, Dikla,

22. Obali, Abimaeli, Sheba,

23. Ofiri, Havila na Yobabu. Hao watu ni wana wa Yoktani.

24. Ukoo wa Abrahamu kutokea Shemu ni kama ifuatavyo: Shemu alimzaa Arpaksadi, naye Arpaksadi akamzaa Shela.

25. Shela akamzaa Eberi, Eberi akamzaa Pelegi, Pelegi akamzaa Reu;

26. Reu akamzaa Serugi, Serugi akamzaa Nahori, Nahori akamzaa Tera,

27. na Tera akamzaa Abramu, ambaye ndiye Abrahamu.

Wazawa wa Ishmaeli

28. Abrahamu alikuwa na watoto wawili wa kiume: Isaka na Ishmaeli.

29. Hivi ndivyo vizazi vyao: Mzaliwa wa kwanza wa Ishmaeli alikuwa Nebayothi na wengine ni Kedari, Adbeeli, Mibsamu,

30. Mishma, Duma, Masa, Hadadi, Tema,

31. Yeturi, Nafishi na Kedema. Hao ndio wana wa Ishmaeli.

32. Abrahamu alikuwa na suria aliyeitwa Ketura. Ketura alimzalia Abrahamu: Zimrani, Yokshani, Medani, Midiani, Ishbaki na Shua. Wana wa Yokshani walikuwa Sheba na Dedani.

33. Wana wa Midiani walikuwa: Efa, Eferi, Henoki, Abida na Eldaa. Wote hao walikuwa wazawa wa Ketura.

Wazawa wa Esau

34. Isaka, mwana wa Abrahamu, alikuwa na wana wawili: Esau na Israeli.

35. Wana wa Esau walikuwa Elifazi, Reueli, Yeushi, Yalamu na Kora.

36. Wana wa Elifazi walikuwa Temani, Omari, Sefo, Gatamu, Kenazi, Timna na Amaleki.

37. Wana wa Reueli walikuwa Nahathi, Zera, Shama na Miza.

Wazawa wa asili wa Edomu

38. Wana wa Seiri walikuwa Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana, Dishoni, Eseri na Dishani.

39. Wana wa Lotani walikuwa wawili: Hori na Homamu. Lotani alikuwa na dada yake aliyeitwa Timna.

40. Wana wa Shobali walikuwa Alvani, Manahathi, Ebali, Shefi na Onamu. Wana wa Sibeoni walikuwa Aya na Ana.

41. Mwana wa Ana alikuwa Dishoni; na wana wa Dishoni walikuwa Hamrani, Eshbani, Ithrani na Kerani.

42. Wana wa Eseri walikuwa Bilhani, Zaawani na Akani; na wana wa Dishoni walikuwa Usi na Arani.

Wafalme wa Edomu

43. Wafuatao ndio wafalme waliotawala nchi ya Edomu kabla mfalme yeyote hajatawala Waisraeli: Bela mwana wa Beori alitawala nchi ya Edomu, akiwa na makao yake makuu katika mji wa Dinhaba.

44. Bela alipofariki, Yobabu mwana wa Zera kutoka Bosra alitawala badala yake.

45. Yobabu alipofariki, Hushamu wa nchi ya Watemi alitawala badala yake.

46. Hushamu alipofariki, Hadadi mwana wa Bedadi alitawala badala yake, makao yake makuu yakiwa katika mji wa Avithi. Huyu ndiye aliyewapiga na kuwashinda Wamidiani katika nchi ya Moabu.

47. Hadadi alipofariki, Samla kutoka Masreka alitawala badala yake.

48. Samla alipofariki, Shauli kutoka Rehobothi ulio karibu na mto Eufrate, alitawala badala yake.

49. Shauli alipofariki, Baal-hanani mwana wa Akbori alitawala badala yake.

50. Baal-hanani alipofariki, Hadadi kutoka Pai alitawala badala yake na jina la mkewe Akbori lilikuwa Mehetabeli, binti Matredi, binti Mezahabu.

51. Naye Hadadi akafariki.Wakuu wa makabila ya Edomu walikuwa Timna, Alva, Yethethi,

52. Oholibama, Ela, Pinoni,

53. Kenazi, Temani, Mibsari,

54. Magdieli na Iramu. Hao ndio wakuu wa makabila ya Edomu.