Agano la Kale

Agano Jipya

Yohane 3:9-15 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Nikodemo akamwuliza, “Mambo haya yanawezekanaje?”

10. Yesu akamjibu, “Je, wewe ni mwalimu katika Israeli na huyajui mambo haya?

11. Kweli nakuambia, sisi twasema tunayoyajua na kushuhudia tuliyoyaona, lakini nyinyi hamkubali ujumbe wetu.

12. Ikiwa nimewaambieni mambo ya kidunia nanyi hamniamini, mtawezaje kuamini nikiwaambieni mambo ya mbinguni?

13. Hakuna mtu aliyepata kwenda juu mbinguni isipokuwa Mwana wa Mtu, ambaye ameshuka kutoka mbinguni.

14. “Kama vile Mose alivyomwinua juu nyoka wa shaba kule jangwani, naye Mwana wa Mtu atainuliwa juu vivyo hivyo,

15. ili kila anayemwamini awe na uhai wa milele.

Kusoma sura kamili Yohane 3