Agano la Kale

Agano Jipya

Yohane 2:2-9 Biblia Habari Njema (BHN)

2. naye Yesu alikuwa amealikwa harusini pamoja na wanafunzi wake.

3. Divai ilipokwisha, mama yake akamwambia, “Hawana divai!”

4. Yesu akamjibu, “Mama, usiniambie la kufanya. Saa yangu bado.”

5. Hapo mama yake akawaambia watumishi, “Lolote atakalowaambieni, fanyeni.”

6. Hapo palikuwa na mitungi sita ya mawe, ambayo kila mmoja uliweza kuchukua kiasi cha madebe mawili au matatu. Ilikuwa imewekwa hapo kufuatana na desturi ya Kiyahudi ya kutawadha.

7. Yesu akawaambia, “Ijazeni mitungi hiyo maji.” Nao wakaijaza mpaka juu.

8. Kisha akawaambia, “Sasa choteni mkampelekee mkuu wa karamu.”

9. Mkuu wa karamu alipoonja hayo maji, kumbe yalikuwa yamegeuka kuwa divai. Yeye hakujua ilikotoka, (lakini wale watumishi waliochota maji walijua). Mkuu wa karamu akamwita bwana arusi,

Kusoma sura kamili Yohane 2