Agano la Kale

Agano Jipya

Yakobo 1:12-18 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Heri mtu anayebaki mwaminifu katika majaribu, kwani akisha stahimili, atapewa tuzo la uhai ambalo Mungu aliwaahidi wale wanaompenda.

13. Kama mtu akijaribiwa, asiseme: “Ninajaribiwa na Mungu.” Maana Mungu hawezi kujaribiwa na uovu, wala yeye hamjaribu mtu yeyote.

14. Lakini mtu hujaribiwa anapovutwa na kunaswa na tamaa zake mbaya.

15. Tamaa ikiiva huzaa dhambi; nayo dhambi ikikomaa huzaa kifo.

16. Ndugu zangu wapenzi, msidanganyike!

17. Kila kipaji chema na kila zawadi kamilifu hutoka mbinguni; hutoka kwa Baba, Muumba wa mianga, ambaye habadiliki wala hana alama yoyote ya ugeugeu.

18. Kwa kupenda kwake mwenyewe alituzaa kwa neno lake la ukweli, ili tuwe katika nafasi ya kwanza miongoni mwa viumbe vyake.

Kusoma sura kamili Yakobo 1