Agano la Kale

Agano Jipya

Waroma 14:7-13 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Maana hakuna mtu yeyote miongoni mwetu aishiye kwa ajili yake mwenyewe, wala hakuna anayekufa kwa ajili yake mwenyewe

8. maana tukiishi twaishi kwa ajili ya Bwana; tukifa, tunakufa kwa ajili ya Bwana. Basi, kama tukiishi au tukifa, sisi ni mali yake Bwana.

9. Maana Kristo alikufa, akafufuka ili apate kuwa Bwana wa walio hai na wafu.

10. Kwa nini basi, wewe wamhukumu ndugu yako? Nawe, kwa nini wamdharau ndugu yako? Sisi sote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu cha Mungu.

11. Maana Maandiko yanasema:“Kama niishivyo, asema Bwana,kila mtu atanipigia magoti,na kila mmoja atakiri kwamba mimi ni Mungu.”

12. Kwa hiyo, kila mmoja wetu atatoa hoja juu yake mwenyewe mbele ya Mungu.

13. Basi, tuache kuhukumiana, bali tuazimie kutokuwa kamwe kikwazo kwa ndugu au kumsababisha aanguke katika dhambi.

Kusoma sura kamili Waroma 14