Agano la Kale

Agano Jipya

Wagalatia 4:10-15 Biblia Habari Njema (BHN)

10. Bado mnaadhimisha siku, miezi na miaka!

11. Nahofu kwamba labda kazi niliyoifanya kwa ajili yenu imepotea bure!

12. Ndugu, nawasihi muwe kama mimi, kwa vile hata mimi nimekuwa kama nyinyi. Hamkunitendea ubaya wowote.

13. Mnajua kwamba ugonjwa wangu ndio ulionipatia fursa ya kuwahubirieni Injili kwa mara ya kwanza.

14. Hata hivyo, wakati ule hamkunidharau wala kunikataa kwa sababu ya udhaifu wangu ingawa mlishawishiwa kufanya hivyo; lakini mlinipokea kama malaika wa Mungu, kama vile ningekuwa Kristo Yesu mwenyewe.

15. Mlikuwa wenye furaha; sasa kumetokea nini? Naapa kwamba wakati ule mngaliweza hata kuyangoa macho yenu na kunipa mimi.

Kusoma sura kamili Wagalatia 4