Agano la Kale

Agano Jipya

Waefeso 5:7-13 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Basi, msishirikiane nao.

8. Zamani nyinyi mlikuwa gizani, lakini sasa nyinyi mko katika mwanga kwa kuungana na Bwana. Ishini kama watoto wa mwanga,

9. maana matokeo ya mwanga ni wema kamili, uadilifu na ukweli.

10. Jaribuni kujua yale yanayompendeza Bwana.

11. Msishiriki katika matendo yasiyofaa ya giza, bali yafichueni.

12. Mambo yanayotendwa kwa siri ni aibu hata kuyataja.

13. Lakini kila kitu kikifichuliwa na mwanga, ukweli wake hudhihirishwa;

Kusoma sura kamili Waefeso 5