Agano la Kale

Agano Jipya

Ufunuo 2:24-29 Biblia Habari Njema (BHN)

24. “Lakini nyinyi wengine mlioko huko Thuatira ambao hamfuati mafundisho yake Yezebeli na ambao hamkujifunza kile wanachokiita Siri ya Shetani, nawaambieni kwamba sitawapeni mzigo mwingine.

25. Lazima mzingatie yale mliyo nayo sasa mpaka nitakapokuja.

26. “Mshindi na mwenye kuzingatia mpaka mwisho mambo ninayotaka, nitampa mamlaka juu ya watu wa mataifa:

27. Atawaongoza kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama vyombo vya udongo.

28. Mimi pia nimepokea mamlaka hayo kutoka kwa Baba yangu. Tena nitampa nyota ya asubuhi.

29. “Aliye na masikio, basi, na ayasikie yale Roho anayoyaambia makanisa!

Kusoma sura kamili Ufunuo 2