Agano la Kale

Agano Jipya

Tito 3:8-15 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Jambo hili ni kweli.Ninakutaka uyatilie mkazo mambo haya, ili wale wanaomwamini Mungu wawe na hamu ya kuutumia wakati wao katika kutenda mema, yaani mambo mazuri na ya kuwafaa watu.

9. Lakini jiepushe na ubishi wa kipumbavu, ugomvi na mabishano juu ya sheria. Mambo hayo hayana faida yoyote na ni ya bure tu.

10. Mtu anayesababisha mafarakano mpe onyo la kwanza na la pili, kisha achana naye.

11. Wajua kwamba mtu wa namna hiyo amepotoka kabisa, na dhambi zake zathibitisha kwamba amekosea.

12. Baada ya kumtuma kwako Artema au Tukiko, fanya bidii kuja Nikopoli unione, maana nimeamua kukaa huko wakati wa majira ya baridi.

13. Jitahidi kumsaidia mwanasheria Zena na Apolo ili waweze kuanza ziara zao, na uhakikishe kwamba wana kila kitu wanachohitaji.

14. Ni lazima watu wetu wajifunze kuutumia wakati wao katika kutenda mema ili wasaidie katika mahitaji ya kweli, na maisha yao yawe ya kufaa.

15. Watu wote walio pamoja nami wanakusalimu. Wasalimu rafiki zetu katika imani.Nawatakieni nyote neema ya Mungu.

Kusoma sura kamili Tito 3