Agano la Kale

Agano Jipya

Mathayo 4:15-25 Biblia Habari Njema (BHN)

15. “Nchi ya Zebuluni na nchi ya Naftali,kuelekea baharini ngambo ya mto Yordani,Galilaya, nchi ya watu wa mataifa!

16. Watu waliokaa gizaniwameona mwanga mkubwa.Nao walioishi katika nchi ya giza na kivuli cha kifo,mwanga umewaangazia!”

17. Tangu wakati huo Yesu alianza kuhubiri akisema, “Tubuni, maana ufalme wa mbinguni umekariia!”

18. Yesu alipokuwa anatembea kando ya ziwa Galilaya, aliwaona ndugu wawili wavuvi; Simoni (aitwaye Petro) na Andrea, ndugu yake; walikuwa wakivua samaki kwa nyavu ziwani.

19. Basi, akawaambia, “Nifuateni, nami nitawafanya nyinyi wavuvi wa watu.”

20. Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.

21. Alipokwenda mbele kidogo, aliwaona ndugu wengine wawili: Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo. Hao walikuwa ndani ya mashua pamoja na baba yao Zebedayo, wakitengeneza nyavu zao. Basi, Yesu akawaita,

22. nao mara wakaiacha mashua pamoja na baba yao, wakamfuata.

23. Yesu alikuwa anakwenda kila mahali wilayani Galilaya, akifundisha katika masunagogi na kuhubiri Habari Njema juu ya ufalme wa Mungu. Aliponya kila namna ya maradhi na magonjwa waliyokuwa nayo watu.

24. Habari zake zikaenea pande zote za Siria. Wagonjwa wote wenye maradhi ya kila namna na wale waliosumbuliwa na kila namna ya taabu: Waliopagawa na pepo, wenye kifafa na watu waliokuwa wamelemaa, walipelekwa kwake; naye akawaponya wote.

25. Makundi mengi ya watu kutoka Galilaya, Dekapoli, Yerusalemu, Yudea na ngambo ya mto Yordani, yalimfuata.

Kusoma sura kamili Mathayo 4