Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28

Agano la Kale

Agano Jipya

Mathayo 4 Biblia Habari Njema (BHN)

Kujaribiwa kwa Yesu

1. Kisha Roho alimwongoza Yesu mpaka jangwani ili ajaribiwe na Ibilisi.

2. Akafunga siku arubaini mchana na usiku, na mwishowe akaona njaa.

3. Basi, mshawishi akamjia, akamwambia, “Ikiwa wewe ni Mwana wa Mungu, amuru mawe haya yawe mikate.”

4. Yesu akamjibu, “Imeandikwa:‘Mtu haishi kwa mkate tu,ila kwa kila neno asemalo Mungu.’”

5. Kisha Ibilisi akamchukua mpaka Yerusalemu, mji mtakatifu, akamweka juu ya mnara wa hekalu,

6. akamwambia, “Ikiwa wewe ni Mwana wa Mungu, jitupe chini; maana imeandikwa:‘Mungu atawaamuru malaika wake kwa ajili yako;watakuchukua mikononi mwao,usije ukajikwaa kwenye jiwe.’”

7. Yesu akamwambia, “Imeandikwa pia:‘Usimjaribu Bwana, Mungu wako.’”

8. Kisha Ibilisi akamchukua mpaka juu ya mlima mrefu, akamwonesha falme zote za ulimwengu na fahari zake,

9. akamwambia, “Hivi vyote nitakupa kama ukipiga magoti na kuniabudu.”

10. Hapo, Yesu akamwambia, “Nenda zako Shetani! Imeandikwa:‘Utamwabudu Bwana Mungu wakona kumtumikia yeye peke yake.’”

11. Basi, Ibilisi akamwacha, na malaika wakaja, wakamhudumia.

Yesu anaanza kazi Galilaya

12. Yesu aliposikia kwamba Yohane ametiwa gerezani alikwenda Galilaya.

13. Aliondoka Nazareti, akaenda Kafarnaumu, mji ulio kando ya bahari ya Genesareti, mpakani mwa wilaya za Zebuluni na Naftali, akakaa huko.

14. Ndivyo lilivyotimia lile neno lililosemwa kwa njia ya nabii Isaya:

15. “Nchi ya Zebuluni na nchi ya Naftali,kuelekea baharini ngambo ya mto Yordani,Galilaya, nchi ya watu wa mataifa!

16. Watu waliokaa gizaniwameona mwanga mkubwa.Nao walioishi katika nchi ya giza na kivuli cha kifo,mwanga umewaangazia!”

17. Tangu wakati huo Yesu alianza kuhubiri akisema, “Tubuni, maana ufalme wa mbinguni umekariia!”

Yesu anawaita wavuvi wanne

18. Yesu alipokuwa anatembea kando ya ziwa Galilaya, aliwaona ndugu wawili wavuvi; Simoni (aitwaye Petro) na Andrea, ndugu yake; walikuwa wakivua samaki kwa nyavu ziwani.

19. Basi, akawaambia, “Nifuateni, nami nitawafanya nyinyi wavuvi wa watu.”

20. Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.

21. Alipokwenda mbele kidogo, aliwaona ndugu wengine wawili: Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo. Hao walikuwa ndani ya mashua pamoja na baba yao Zebedayo, wakitengeneza nyavu zao. Basi, Yesu akawaita,

22. nao mara wakaiacha mashua pamoja na baba yao, wakamfuata.

Yesu anafundisha watu na kuponya wagonjwa

23. Yesu alikuwa anakwenda kila mahali wilayani Galilaya, akifundisha katika masunagogi na kuhubiri Habari Njema juu ya ufalme wa Mungu. Aliponya kila namna ya maradhi na magonjwa waliyokuwa nayo watu.

24. Habari zake zikaenea pande zote za Siria. Wagonjwa wote wenye maradhi ya kila namna na wale waliosumbuliwa na kila namna ya taabu: Waliopagawa na pepo, wenye kifafa na watu waliokuwa wamelemaa, walipelekwa kwake; naye akawaponya wote.

25. Makundi mengi ya watu kutoka Galilaya, Dekapoli, Yerusalemu, Yudea na ngambo ya mto Yordani, yalimfuata.