Agano la Kale

Agano Jipya

Mathayo 26:42-46 Biblia Habari Njema (BHN)

42. Akaenda tena mara ya pili akasali: “Baba yangu, kama haiwezekani kikombe hiki kipite bila mimi kukinywa, basi, utakalo lifanyike.”

43. Akawaendea tena, akawakuta wamelala, maana macho yao yalikuwa yamebanwa na usingizi.

44. Basi, akawaacha, akaenda tena kusali mara ya tatu kwa maneno yaleyale.

45. Kisha akawaendea wale wanafunzi, akawaambia, “Je, mngali mmelala na kupumzika? Tazameni! Saa yenyewe imefika, na Mwana wa Mtu atatolewa kwa watu wenye dhambi.

46. Amkeni; twendeni zetu. Tazameni! Anakuja yule atakayenisaliti.”

Kusoma sura kamili Mathayo 26