Agano la Kale

Agano Jipya

Mathayo 26:23-26 Biblia Habari Njema (BHN)

23. Yesu akajibu, “Anayechovya mkate pamoja nami katika bakuli ndiye atakayenisaliti.

24. Naam, Mwana wa Mtu anakwenda zake kama Maandiko Matakatifu yasemavyo, lakini ole wake mtu yule atakayemsaliti Mwana wa Mtu! Ingalikuwa afadhali kwa mtu huyo kama hangalizaliwa.”

25. Yuda, ambaye ndiye aliyetaka kumsaliti, akamwuliza, “Mwalimu! Je, ni mimi?” Yesu akamjibu, “Wewe umesema.”

26. Walipokuwa wanakula, Yesu akatwaa mkate, akamshukuru Mungu, akaumega, akawapa wanafunzi wake akisema, “Twaeni mle; huu ni mwili wangu.”

Kusoma sura kamili Mathayo 26