Agano la Kale

Agano Jipya

Mathayo 26:19-33 Biblia Habari Njema (BHN)

19. Wanafunzi wakafanya kama Yesu alivyowaagiza, wakaandaa Pasaka.

20. Kulipokuwa jioni, Yesu akakaa mezani pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili.

21. Walipokuwa wakila, Yesu akasema, “Nawaambieni kweli, mmoja wenu atanisaliti.”

22. Wanafunzi wakahuzunika sana, wakaanza kuuliza mmojammoja, “Bwana! Je, ni mimi?”

23. Yesu akajibu, “Anayechovya mkate pamoja nami katika bakuli ndiye atakayenisaliti.

24. Naam, Mwana wa Mtu anakwenda zake kama Maandiko Matakatifu yasemavyo, lakini ole wake mtu yule atakayemsaliti Mwana wa Mtu! Ingalikuwa afadhali kwa mtu huyo kama hangalizaliwa.”

25. Yuda, ambaye ndiye aliyetaka kumsaliti, akamwuliza, “Mwalimu! Je, ni mimi?” Yesu akamjibu, “Wewe umesema.”

26. Walipokuwa wanakula, Yesu akatwaa mkate, akamshukuru Mungu, akaumega, akawapa wanafunzi wake akisema, “Twaeni mle; huu ni mwili wangu.”

27. Kisha akatwaa kikombe cha divai, akashukuru, akawapa akisema, “Kunyweni nyote;

28. maana hii ni damu yangu inayothibitisha agano, damu inayomwagwa kwa ajili ya watu wengi ili kuwaondolea dhambi.

29. Nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka siku ile nitakapoinywa mpya pamoja nanyi katika ufalme wa Baba yangu.”

30. Baada ya kuimba wimbo, wakaondoka, wakaenda katika mlima wa Mizeituni.

31. Kisha Yesu akawaambia, “Usiku huu wa leo, nyinyi nyote mtakuwa na mashaka nami, maana Maandiko Matakatifu yasema:‘Nitampiga mchungaji,na kondoo wa kundi watatawanyika.’

32. Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulieni Galilaya.”

33. Petro akamwambia Yesu, “Hata kama wote watakuwa na mashaka nawe na kukuacha, mimi sitakuacha kamwe.”

Kusoma sura kamili Mathayo 26