Agano la Kale

Agano Jipya

Mathayo 15:12-21 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Kisha wanafunzi wakamwendea, wakamwambia, “Je, unajua kwamba Mafarisayo walichukizwa waliposikia maneno yako?”

13. Lakini yeye akawajibu, “Kila mmea ambao Baba yangu aliye mbinguni hakupanda, utangolewa.

14. Waacheni wenyewe! Wao ni vipofu, viongozi wa vipofu; na kipofu akimwongoza kipofu, wote wawili hutumbukia shimoni.”

15. Petro akasema, “Tufafanulie huo mfano.”

16. Yesu akasema, “Hata nyinyi hamwelewi?

17. Je, hamwelewi kwamba kila kinachoingia kinywani huenda tumboni na baadaye hutolewa nje chooni?

18. Lakini mambo yatokayo kinywani hutoka moyoni, na hayo ndiyo yanayomtia mtu unajisi.

19. Maana moyoni hutoka mawazo ya uuaji, uzinzi, uasherati, wizi, ushahidi wa uongo na kashfa.

20. Hayo ndiyo yanayomtia mtu unajisi. Lakini kula chakula bila kunawa mikono hakumtii mtu unajisi.”

21. Yesu aliondoka mahali hapo akaenda kukaa katika sehemu za Tiro na Sidoni.

Kusoma sura kamili Mathayo 15