Agano la Kale

Agano Jipya

Matendo 28:18-27 Biblia Habari Njema (BHN)

18. Waliponihoji na kuona kwamba sikuwa na hatia yoyote, walitaka kuniachia.

19. Lakini Wayahudi wengine walipinga jambo hilo, nami nikalazimika kukata rufani kwa Kaisari, ingawa sikuwa na chochote cha kuwashtaki wananchi wenzangu.

20. Ni kwa sababu hiyo nimeomba kuonana na kuongea nanyi, maana nimefungwa minyororo hii kwa sababu ya tumaini lile la Israeli.”

21. Wao wakamwambia, “Sisi hatujapokea barua yoyote kutoka Yudea, wala hakuna ndugu yeyote aliyefika hapa na kutoa habari rasmi au kusema chochote kibaya juu yako.

22. Lakini tunafikiri inafaa tusikie kutoka kwako mwenyewe mambo yaliyo kichwani mwako. Kwa maana tujualo sisi kuhusu hicho kikundi ni kwamba kinapingwa kila mahali.”

23. Basi, walipanga naye siku kamili ya kukutana, na wengi wakafika huko alikokuwa anakaa. Tangu asubuhi mpaka jioni Paulo aliwaeleza na kuwafafanulia juu ya ufalme wa Mungu, akijaribu kuwafanya wakubali habari juu ya Yesu kwa kutumia sheria na maandiko ya manabii.

24. Baadhi yao walikubali maneno yake, lakini wengine hawakuamini.

25. Basi, kukawa na mtengano wa fikira kati yao. Walipokuwa wanakwenda zao, Paulo alisema jambo hili: “Kweli ni sawa yale Roho Mtakatifu aliyowaarifu wazee wenu kwa njia ya nabii Isaya

26. akisema:‘Nenda kwa watu hawa ukawaambie:Kusikia mtasikia, lakini hamtaelewa;kutazama mtatazama, lakini hamtaona.

27. Maana akili za watu hawa zimepumbaa,wameziba masikio yao,wamefumba macho yao.La sivyo, wangeona kwa macho yao,wangesikia kwa masikio yao.Wangeelewa kwa akili zao,na kunigeukia, asema Bwana,nami ningewaponya.’”

Kusoma sura kamili Matendo 28