Agano la Kale

Agano Jipya

Matendo 21:5-10 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Lakini muda wetu ulipokwisha tuliondoka. Wote pamoja na wanawake na watoto wao walitusindikiza mpaka nje ya mji. Tulipofika pwani, sote tulipiga magoti tukasali.

6. Kisha tuliagana; sisi tukapanda meli, nao wakarudi makwao.

7. Sisi tuliendelea na safari yetu kutoka Tiro tukafika Tolemai ambapo tuliwasalimu ndugu zetu, tukakaa nao siku moja.

8. Kesho yake tuliondoka tukaenda Kaisarea. Huko tulikwenda nyumbani kwa mhubiri Filipo. Yeye alikuwa mmoja wa wale saba waliochaguliwa kule Yerusalemu.

9. Alikuwa na binti wanne ambao walikuwa na kipaji cha unabii.

10. Baada ya kukaa huko siku kadhaa, nabii mmoja aitwaye Agabo alifika kutoka Yudea.

Kusoma sura kamili Matendo 21