Agano la Kale

Agano Jipya

Matendo 2:12-18 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Wote walishangaa na kufadhaika huku wakiulizana, “Hii ina maana gani?”

13. Lakini wengine wakawadhihaki wakisema, “Watu hawa wamelewa divai mpya!”

14. Lakini Petro alisimama pamoja na wale kumi na mmoja akaanza kuwahutubia watu kwa sauti kubwa: “Ndugu Wayahudi nanyi nyote mnaokaa hapa Yerusalemu, sikilizeni kwa makini maneno yangu.

15. Watu hawa hawakulewa kama mnavyodhani; mbona ni saa tatu tu asubuhi?

16. Ukweli ni kwamba jambo hili ni lile alilosema nabii Yoeli:

17. ‘Katika siku zile za mwisho, asema Bwana,nitawamiminia binadamu wote Roho wangu.Watoto wenu wa kiume na wa kike watatoa unabii,vijana wenu wataona maono,na wazee wenu wataota ndoto.

18. Naam, hata watumishi wangu wa kiume na kike,nitawamiminia Roho wangu siku zile,nao watatoa unabii.

Kusoma sura kamili Matendo 2