Agano la Kale

Agano Jipya

Matendo 2:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Siku ya Pentekoste ilipofika, waumini wote walikuwa wamekusanyika mahali pamoja.

2. Ghafla, sauti ikasikika kutoka angani; sauti iliyokuwa kama ya upepo mkali, ikaijaza ile nyumba yote walimokuwa wamekaa.

3. Kisha, vikatokea vitu vilivyoonekana kama ndimi za moto, vikagawanyika na kutua juu ya kila mmoja wao.

4. Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema lugha mbalimbali kadiri Roho alivyowawezesha.

5. Na huko Yerusalemu walikuwako Wayahudi, watu wamchao Mungu, waliotoka katika kila nchi duniani.

Kusoma sura kamili Matendo 2