Agano la Kale

Agano Jipya

Matendo 15:5-9 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Lakini waumini wengine waliokuwa wa kikundi cha Mafarisayo walisimama, wakasema, “Ni lazima watu wa mataifa mengine watahiriwe na kufundishwa kuifuata sheria.”

6. Basi, mitume na wazee walifanya mkutano maalumu wa kuchunguza jambo hilo.

7. Baada ya majadiliano marefu, Petro alisimama, akasema, “Ndugu zangu, nyinyi mnafahamu kwamba hapo awali Mungu alipenda kunichagua mimi miongoni mwenu nitangaze Habari Njema kwa watu wa mataifa, wapate kusikia na kuamini.

8. Naye Mungu anayejua mioyo ya watu, alithibitisha kwamba amewakubali kwa kuwapa nao Roho Mtakatifu kama alivyotupa sisi.

9. Hakufanya ubaguzi wowote kati yetu na wao; aliitakasa mioyo yao kwa imani.

Kusoma sura kamili Matendo 15