Agano la Kale

Agano Jipya

Matendo 13:36-43 Biblia Habari Njema (BHN)

36. Sasa, Daudi mwenyewe alitimiza matakwa ya Mungu wakati wake; kisha akafa na kuzikwa karibu na wazee wake, na mwili wake ukaoza.

37. Lakini yule ambaye Mungu alimfufua kutoka wafu hakupata kuoza.

38. Kwa hiyo, jueni, ndugu zangu, kwamba kwa njia ya mtu huyu ujumbe kuhusu kusamehewa dhambi unahubiriwa kwenu;

39. na ya kwamba kila mmoja anayemwamini Yesu anasamehewa dhambi zote, jambo ambalo halingewezekana kwa njia ya sheria.

40. Jihadharini basi, msije mkapatwa na yale yaliyosemwa na manabii:

41. ‘Sikilizeni enyi wenye madharau,shangaeni mpotee!Kwa maana kitu ninachofanya sasa, nyakati zenu,ni kitu ambacho hamtakiamini hata kama mtu akiwaelezeni.’”

42. Paulo na Barnaba walipokuwa wanatoka katika lile sunagogi, wale watu waliwaalika waje tena siku ya Sabato iliyofuata, waongee zaidi juu ya mambo hayo.

43. Mkutano huo ulipomalizika, Wayahudi wengi na watu wa mataifa mengine waliokuwa wameongokea dini ya Kiyahudi waliwafuata Paulo na Barnaba. Hao mitume waliongea nao, wakawatia moyo waendelee kuishi wakitegemea neema ya Mungu.

Kusoma sura kamili Matendo 13