Agano la Kale

Agano Jipya

Matendo 12:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Karibu wakati huohuo, mfalme Herode alianza kuwatesa baadhi ya Wakristo.

2. Alimuua kwa upanga Yakobo, ndugu yake Yohane.

3. Alipoona kuwa kitendo hicho kiliwapendeza Wayahudi, aliendelea, akamkamata Petro. (Hiyo ilifanyika wakati wa sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu).

4. Baada ya kutiwa nguvuni, Petro alifungwa gerezani, akawekwa chini ya ulinzi wa vikundi vinne vya askari wannewanne. Herode alikusudia kumtoa hadharani baada ya sikukuu ya Pasaka.

5. Basi, Petro alipokuwa gerezani, kanisa lilikuwa linamwombea kwa Mungu kwa moyo.

Kusoma sura kamili Matendo 12