Agano la Kale

Agano Jipya

Marko 3:8-14 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Idumea, ngambo ya mto Yordani, Tiro na Sidoni. Watu hao wengi walimwendea Yesu kwa sababu ya kusikia mambo mengi aliyokuwa ameyatenda.

9. Yesu akawaambia wanafunzi wake wamtayarishie mashua moja, ili umati wa watu usije ukamsonga.

10. Alikuwa amewaponya watu wengi, na wagonjwa wote wakawa wanamsonga ili wapate kumgusa.

11. Na watu waliokuwa wamepagawa na pepo wachafu walipomwona, walijitupa chini mbele yake na kupaza sauti, “Wewe ni Mwana wa Mungu!”

12. Lakini Yesu akawaamuru kwa ukali wasimjulishe kwa watu.

13. Yesu alipanda kilimani, akawaita wale aliowataka. Basi, wakamwendea,

14. naye akawateua watu kumi na wawili ambao aliwaita mitume, wakae naye, awatume kuhubiri

Kusoma sura kamili Marko 3