Agano la Kale

Agano Jipya

Marko 3:28-35 Biblia Habari Njema (BHN)

28. “Kweli nawaambieni, watu watasamehewa dhambi zao zote na kufuru zao zote;

29. lakini anayesema mabaya dhidi ya Roho Mtakatifu, hatasamehewa kamwe; ana hatia ya dhambi ya milele.” (

30. Yesu alisema hivyo kwa sababu walikuwa wanasema, “Ana pepo mchafu.”)

31. Mama yake Yesu na ndugu zake walifika hapo, wakasimama nje, wakampelekea ujumbe kumwita.

32. Umati wa watu ulikuwa umekaa hapo kumzunguka. Basi, watu wakamwambia, “Mama yako na ndugu zako wako nje, wanataka kukuona.”

33. Yesu akawaambia, “Mama yangu na ndugu zangu ni kina nani?”

34. Hapo akawatazama watu waliokuwa wamemzunguka, akasema, “Tazameni! Hawa ndio mama yangu na ndugu zangu.

35. Mtu yeyote anayefanya anayotaka Mungu, huyo ndiye kaka yangu, dada yangu na mama yangu.”

Kusoma sura kamili Marko 3