Agano la Kale

Agano Jipya

Marko 15:6-13 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Kila wakati wa sikukuu ya Pasaka, Pilato alikuwa na desturi ya kuwafungulia mfungwa mmoja waliyemtaka.

7. Basi, kulikuwa na mtu mmoja aitwaye Baraba, ambaye alikuwa amefungwa pamoja na waasi wengine kwa kusababisha uasi na mauaji.

8. Watu wengi wakamwendea Pilato wakamwomba awafanyie kama kawaida yake.

9. Pilato akawauliza, “Je, mwataka niwafungulieni Mfalme wa Wayahudi?”

10. Alisema hivyo kwa sababu alijua wazi kwamba makuhani wakuu walimkabidhi Yesu kwake kwa sababu ya wivu.

11. Lakini makuhani wakuu wakawachochea watu wamwombe Pilato awafungulie Baraba.

12. Pilato akawauliza tena, “Basi, sasa mwataka nifanye nini na mtu huyu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?”

13. Watu wote wakapaza sauti tena: “Msulubishe!”

Kusoma sura kamili Marko 15