Agano la Kale

Agano Jipya

Marko 15:1-14 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Kulipopambazuka, makuhani wakuu walifanya shauri pamoja na wazee, waalimu wa sheria na Baraza lote, wakamfunga Yesu pingu, wakampeleka na kumkabidhi kwa Pilato.

2. Pilato akamwuliza Yesu, “Je, wewe ni Mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe umesema.”

3. Makuhani wakuu wakamshtaki Yesu mambo mengi.

4. Pilato akamwuliza tena Yesu, “Je, hujibu neno? Tazama wanavyotoa mashtaka mengi juu yako.”

5. Lakini Yesu hakujibu neno, hata Pilato akashangaa.

6. Kila wakati wa sikukuu ya Pasaka, Pilato alikuwa na desturi ya kuwafungulia mfungwa mmoja waliyemtaka.

7. Basi, kulikuwa na mtu mmoja aitwaye Baraba, ambaye alikuwa amefungwa pamoja na waasi wengine kwa kusababisha uasi na mauaji.

8. Watu wengi wakamwendea Pilato wakamwomba awafanyie kama kawaida yake.

9. Pilato akawauliza, “Je, mwataka niwafungulieni Mfalme wa Wayahudi?”

10. Alisema hivyo kwa sababu alijua wazi kwamba makuhani wakuu walimkabidhi Yesu kwake kwa sababu ya wivu.

11. Lakini makuhani wakuu wakawachochea watu wamwombe Pilato awafungulie Baraba.

12. Pilato akawauliza tena, “Basi, sasa mwataka nifanye nini na mtu huyu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?”

13. Watu wote wakapaza sauti tena: “Msulubishe!”

14. Lakini Pilato akawauliza, “Kwa nini! Amefanya ubaya gani?” Lakini wao wakazidi kupaza sauti, “Msulubishe!”

Kusoma sura kamili Marko 15