Agano la Kale

Agano Jipya

Marko 12:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Yesu alianza kusema nao kwa mifano: “Mtu mmoja alilima shamba la mizabibu. Akalizungushia ukuta, na katikati yake akachimba kisima cha kusindikia divai, akajenga mnara pia. Akalikodisha shamba hilo kwa wakulima, akasafiri hadi nchi ya mbali.

2. Wakati wa mavuno, alimtuma mtumishi wake kwa wale wakulima, akamletee sehemu ya mazao ya shamba lake.

3. Wale wakulima wakamkamata, wakampiga, wakamrudisha mikono mitupu.

4. Akamtuma tena mtumishi mwingine; huyu pia wakamwumiza kichwa na kumtendea vibaya.

Kusoma sura kamili Marko 12