Agano la Kale

Agano Jipya

Marko 11:16-22 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Hakumruhusu mtu yeyote kupitia hekaluni akichukua kitu.

17. Kisha akawafundisha, “Imeandikwa: ‘Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa ajili ya mataifa yote!’ Lakini nyinyi mmeifanya kuwa pango la wanyanganyi!”

18. Makuhani wakuu na waalimu wa sheria waliposikia hayo, walianza kutafuta njia ya kumwangamiza. Lakini walimwogopa kwa sababu umati wa watu ulishangazwa na mafundisho yake.

19. Ilipokuwa jioni, Yesu na wanafunzi wake waliondoka mjini.

20. Asubuhi na mapema, walipokuwa wanapita, waliuona ule mtini umenyauka wote, hata mizizi.

21. Petro aliukumbuka, akamwambia Yesu, “Mwalimu, tazama! Ule mtini ulioulaani, umenyauka!”

22. Yesu akawaambia, “Mwaminini Mungu.

Kusoma sura kamili Marko 11