Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 4:8-25 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Yesu akamjibu, “Imeandikwa:‘Utamwabudu Bwana Mungu wako,na kumtumikia yeye peke yake.’”

9. Ibilisi akamchukua mpaka Yerusalemu, kwenye mnara wa hekalu, akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, jitupe chini

10. kwa maana imeandikwa:‘Atawaamuru malaika wake wakulinde,’

11. na tena,‘Watakuchukua mikononi mwao,usije ukajikwaa mguu kwenye jiwe.’”

12. Lakini Yesu akamjibu, “Imeandikwa: ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’”

13. Ibilisi alipokwisha mjaribu kwa kila njia, akamwacha kwa muda.

14. Hapo Yesu alirudi Galilaya akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, na habari zake zikaenea katika sehemu zote za jirani.

15. Naye akawa anawafundisha watu katika masunagogi yao, akasifiwa na wote.

16. Basi, Yesu alikwenda Nazareti, mahali alipolelewa, na siku ya Sabato, aliingia katika sunagogi kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome Maandiko Matakatifu kwa sauti.

17. Akapokea kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na akakuta mahali palipoandikwa:

18. “Roho wa Bwana yu juu yangu,kwani ameniweka wakfuniwaletee maskini Habari Njema.Amenituma niwatangazie mateka uhuru wao,na vipofu watapata kuona tena;amenituma niwakomboe wanaoonewa,

19. na kutangaza mwaka wa neema ya Bwana.”

20. Baada ya kusoma, akafunga kile kitabu, akampa mtumishi, kisha akaketi; watu wote wakamkodolea macho.

21. Naye akaanza kuwaambia, “Andiko hili mlilosikia limetimia leo.”

22. Wote wakavutiwa sana naye, wakastaajabia maneno mazuri aliyosema. Wakasema, “Je, huyu si mwana wa Yosefu?”

23. Naye akawaambia, “Bila shaka mtaniambia msemo huu: ‘Mganga jiponye mwenyewe,’ na pia mtasema: ‘Yote tuliyosikia umeyafanya kule Kafarnaumu, yafanye pia hapa kijijini mwako.’”

24. Akaendelea kusema, “Hakika nawaambieni, nabii hatambuliwi kijijini mwake.

25. Lakini, sikilizeni! Kweli kulikuwa na wajane wengi katika nchi ya Israeli nyakati za Elia. Wakati huo mvua iliacha kunyesha kwa muda wa miaka mitatu na nusu; kukawa na njaa kubwa katika nchi yote.

Kusoma sura kamili Luka 4