Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 4:19-22 Biblia Habari Njema (BHN)

19. na kutangaza mwaka wa neema ya Bwana.”

20. Baada ya kusoma, akafunga kile kitabu, akampa mtumishi, kisha akaketi; watu wote wakamkodolea macho.

21. Naye akaanza kuwaambia, “Andiko hili mlilosikia limetimia leo.”

22. Wote wakavutiwa sana naye, wakastaajabia maneno mazuri aliyosema. Wakasema, “Je, huyu si mwana wa Yosefu?”

Kusoma sura kamili Luka 4