Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 4:16-21 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Basi, Yesu alikwenda Nazareti, mahali alipolelewa, na siku ya Sabato, aliingia katika sunagogi kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome Maandiko Matakatifu kwa sauti.

17. Akapokea kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na akakuta mahali palipoandikwa:

18. “Roho wa Bwana yu juu yangu,kwani ameniweka wakfuniwaletee maskini Habari Njema.Amenituma niwatangazie mateka uhuru wao,na vipofu watapata kuona tena;amenituma niwakomboe wanaoonewa,

19. na kutangaza mwaka wa neema ya Bwana.”

20. Baada ya kusoma, akafunga kile kitabu, akampa mtumishi, kisha akaketi; watu wote wakamkodolea macho.

21. Naye akaanza kuwaambia, “Andiko hili mlilosikia limetimia leo.”

Kusoma sura kamili Luka 4