Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 4:13-23 Biblia Habari Njema (BHN)

13. Ibilisi alipokwisha mjaribu kwa kila njia, akamwacha kwa muda.

14. Hapo Yesu alirudi Galilaya akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, na habari zake zikaenea katika sehemu zote za jirani.

15. Naye akawa anawafundisha watu katika masunagogi yao, akasifiwa na wote.

16. Basi, Yesu alikwenda Nazareti, mahali alipolelewa, na siku ya Sabato, aliingia katika sunagogi kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome Maandiko Matakatifu kwa sauti.

17. Akapokea kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na akakuta mahali palipoandikwa:

18. “Roho wa Bwana yu juu yangu,kwani ameniweka wakfuniwaletee maskini Habari Njema.Amenituma niwatangazie mateka uhuru wao,na vipofu watapata kuona tena;amenituma niwakomboe wanaoonewa,

19. na kutangaza mwaka wa neema ya Bwana.”

20. Baada ya kusoma, akafunga kile kitabu, akampa mtumishi, kisha akaketi; watu wote wakamkodolea macho.

21. Naye akaanza kuwaambia, “Andiko hili mlilosikia limetimia leo.”

22. Wote wakavutiwa sana naye, wakastaajabia maneno mazuri aliyosema. Wakasema, “Je, huyu si mwana wa Yosefu?”

23. Naye akawaambia, “Bila shaka mtaniambia msemo huu: ‘Mganga jiponye mwenyewe,’ na pia mtasema: ‘Yote tuliyosikia umeyafanya kule Kafarnaumu, yafanye pia hapa kijijini mwako.’”

Kusoma sura kamili Luka 4