Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 23:12-19 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Herode na Pilato, ambao hapo awali walikuwa maadui, tangu siku hiyo wakawa marafiki.

13. Basi, Pilato akaitisha mkutano wa makuhani wakuu, viongozi na watu,

14. akawaambia, “Mmemleta mtu huyu kwangu mkisema kwamba alikuwa anawapotosha watu. Sasa sikilizeni! Baada ya kuchunguza jambo hilo mbele yenu, sikumpata na kosa lolote kuhusu mashtaka yenu juu yake.

15. Wala si mimi tu, bali hata Herode hakuona kosa lolote, kwa maana amemrudisha kwangu. Ni dhahiri kwamba mtu huyu hakufanya chochote kinachostahili adhabu ya kifo.

16. Hivyo, nitaamuru apigwe viboko, halafu nitamwachilia.” [

17. Kila sikukuu ya Pasaka, ilimlazimu Pilato kuwafungulia mfungwa mmoja.]

18. Lakini wote wakapiga kelele pamoja: “Mwondoe huyo, utufungulie Baraba!” (

19. Baraba alikuwa ametiwa ndani kwa kusababisha uasi katika mji na pia kwa sababu ya kuua.)

Kusoma sura kamili Luka 23