Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 20:3-10 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Yesu akawaambia, “Na mimi nitawaulizeni swali:

4. Mamlaka ya Yohane ya kubatiza yalitoka kwa Mungu au kwa watu?”

5. Lakini wao wakajadiliana hivi: “Tukisema yalitoka kwa Mungu, yeye atatuuliza: ‘Mbona hamkumsadiki?’

6. Na tukisema yalitoka kwa binadamu, watu wote hapa watatupiga mawe, maana wote wanaamini kwamba Yohane alikuwa nabii.”

7. Basi, wakamwambia, “Hatujui mamlaka hayo yalitoka wapi.”

8. Yesu akawaambia, “Hata mimi sitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani.”

9. Yesu akaendelea kuwaambia watu mfano huu: “Mtu mmoja alilima shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima; kisha akasafiri hadi nchi ya mbali, akakaa huko kwa muda mrefu.

10. Wakati wa mavuno, mtu huyo alimtuma mtumishi wake kwa wale wakulima, akachukue sehemu ya matunda ya shamba la mizabibu. Lakini wale wakulima wakampiga mtumishi huyo, wakamrudisha mikono mitupu.

Kusoma sura kamili Luka 20