Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 2:30-37 Biblia Habari Njema (BHN)

30. Maana kwa macho yangu nimeuona wokovu ulioleta,

31. ambao umeutayarisha uonekane na watu wote:

32. Mwanga utakaowaangazia watu wa mataifa,na utukufu kwa watu wako Israeli.”

33. Baba yake Yesu na mama yake walikuwa wakistaajabia maneno aliyosema Simeoni juu ya mtoto.

34. Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, “Mtoto huyu atakuwa sababu ya kupotea na kuokoka kwa watu wengi katika Israeli. Naye atakuwa ishara itakayopingwa na watu;

35. na hivyo mawazo ya watu wengi yataonekana wazi. Nawe mwenyewe, uchungu ulio kama upanga mkali utauchoma moyo wako.”

36. Palikuwa na nabii mmoja mwanamke, mzee sana, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa ameishi na mumewe kwa miaka saba tangu alipoolewa.

37. Halafu alibaki mjane hadi wakati huo akiwa mzee wa miaka themanini na minne. Wakati huo wote alikaa hekaluni akifunga na kusali usiku na mchana.

Kusoma sura kamili Luka 2