Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 17:25-30 Biblia Habari Njema (BHN)

25. Lakini kabla ya hayo, itambidi ateseke sana na kukataliwa na kizazi hiki.

26. Kama ilivyokuwa nyakati za Noa, ndivyo itakavyokuwa katika siku za Mwana wa Mtu.

27. Watu waliendelea kula na kunywa, kuoa na kuolewa mpaka wakati ule Noa alipoingia katika safina. Gharika ikatokea na kuwaangamiza wote.

28. Itakuwa kama ilivyotokea wakati wa Loti. Watu waliendelea kula na kunywa, kununua na kuuza, kupanda mbegu na kujenga.

29. Lakini siku ile Loti alipoondoka Sodoma, moto na madini ya kiberiti vikanyesha kama mvua kutoka mbinguni na kuwaangamiza wote.

30. Ndivyo itakavyokuwa siku ile Mwana wa Mtu atakapofunuliwa.

Kusoma sura kamili Luka 17