15. Akaomba kazi kwa mwananchi mmoja wa huko naye akampeleka shambani mwake kulisha nguruwe.
16. Alitamani kula maganda waliyokula wale nguruwe, ila hakuna mtu aliyempa kitu.
17. Alipoanza kupata akili, akafikiri: ‘Mbona kuna wafanyakazi wengi wa baba yangu wanaokula na kusaza, nami ninakufa njaa?
18. Nitarudi kwa baba yangu na kumwambia: Baba, nimemkosea Mungu, na nimekukosea wewe pia.
19. Sistahili hata kuitwa mwanao. Nifanye kama mmoja wa wafanyakazi wako.’