Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 14:30-35 Biblia Habari Njema (BHN)

30. wakisema: ‘Mtu huyu alianza kujenga, lakini hakumalizia.’

31. “Au, ni mfalme gani ambaye akitaka kwenda kupigana na mfalme mwingine, hataketi kwanza na kufikiri kama ataweza, kwa askari wake10,000, kumkabili yule aliye na askari 20,000?

32. Kama anaona hataweza, atawatuma wajumbe kutaka masharti ya amani wakati mfalme huyo mwingine angali mbali.

33. Vivyo hivyo, basi, hakuna hata mmoja wenu atakayekuwa mwanafunzi wangu kama asipoachilia kila kitu alicho nacho.

34. “Chumvi ni nzuri; lakini ikipoteza ladha yake, itakolezwa na nini?

35. Haifai kitu wala kwa udongo wala kwa mbolea. Watu huitupilia mbali. Mwenye masikio na asikie!”

Kusoma sura kamili Luka 14