Agano la Kale

Agano Jipya

1 Yohane 5:7-12 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Basi, wako mashahidi watatu:

8. Roho, maji na damu; na ushahidi wa hawa watatu waafikiana.

9. Ikiwa twaukubali ushahidi wa binadamu, ushahidi wa Mungu una uzito zaidi; na huu ndio ushahidi alioutoa Mungu mwenyewe juu ya Mwanae.

10. Anayemwamini Mwana wa Mungu anao ushahidi huo ndani yake; lakini asiyemwamini Mungu, anamfanya yeye kuwa mwongo, maana hakuamini ushahidi alioutoa Mungu juu ya Mwanae.

11. Na, ushahidi wenyewe ndio huu: Mungu alitupatia uhai wa milele, na uhai huo uko kwa Bwana.

12. Yeyote aliye na Mwana wa Mungu anao uhai huo; asiye na Mwana wa Mungu, hana uhai.

Kusoma sura kamili 1 Yohane 5