Agano la Kale

Agano Jipya

1 Yohane 2:12-15 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Ninawaandikieni nyinyi watoto kwa kuwa dhambi zenu zimeondolewa kwa jina la Kristo.

13. Nawaandikieni nyinyi kina baba kwani mnamjua yeye ambaye amekuwako tangu mwanzo.Nawaandikieni nyinyi vijana kwa sababu mmemshinda yule Mwovu.

14. Nawaandikieni nyinyi watoto kwa sababu mnamjua Baba.Nawaandikieni nyinyi kina baba kwa kuwa mnamjua yeye ambaye amekuwako tangu mwanzo.Nawaandikieni nyinyi vijana kwa sababu mna nguvu;neno la Mungu limo ndani yenuna mumemshinda yule Mwovu.

15. Msiupende ulimwengu, wala chochote kilicho cha ulimwengu. Mtu anayeupenda ulimwengu, upendo wa Baba hauwezi kuwamo ndani yake.

Kusoma sura kamili 1 Yohane 2