Agano la Kale

Agano Jipya

1 Yohane 2:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Watoto wangu, ninawaandikieni mambo haya, kusudi msitende dhambi. Lakini, ikijatokea mtu akatenda dhambi, tunaye mmoja ambaye hutuombea kwa Baba, ndiye Yesu Kristo aliye mwadilifu kabisa.

2. Kristo ndiye sadaka iondoayo dhambi zetu; wala si dhambi zetu sisi tu, bali pia dhambi za ulimwengu wote.

3. Tukizitii amri za Mungu, basi, tunaweza kuwa na hakika kwamba tunamjua.

4. Mtu akisema kwamba anamjua, lakini hazitii amri zake, basi mtu huyo ni mwongo, na ukweli haumo ndani yake.

Kusoma sura kamili 1 Yohane 2