Agano la Kale

Agano Jipya

1 Wakorintho 1:28-31 Biblia Habari Njema (BHN)

28. Mungu ameyachagua yale ambayo kwa fikira za dunia ni mambo yaliyo duni na yanayodharauliwa, mambo ambayo hata hayakuwako, ili kwa hayo ayafutilie mbali yale ambayo kwa fikira za binadamu ni mambo ya maana.

29. Basi, hakuna mtu awezaye kujivunia chochote mbele ya Mungu.

30. Mungu mwenyewe ndiye aliyewaunganisha nyinyi na Kristo Yesu. Mungu amemfanya Kristo awe hekima yetu; kwa njia yake sisi tunapatanishwa na Mungu, tunakuwa watu wake Mungu na kukombolewa.

31. Basi, kama yasemavyo Maandiko Matakatifu:“Mwenye kutaka kujivuna,na ajivunie kazi ya Bwana.”

Kusoma sura kamili 1 Wakorintho 1