1. Dhambi huongea na mtu mwovu,ndani kabisa moyoni mwake;jambo la kumcha Mungu halimo kabisa kwake.
2. Mwovu hujipendelea mwenyewe,hufikiri uovu wake hautagunduliwa na kulaaniwa.
3. Kila asemacho ni uovu na uongo;ameacha kutumia hekima na kutenda mema.
4. Alalapo huwaza kutenda maovu,hujiweka katika njia isiyo njema,wala haachani na uovu.
5. Fadhili zako ee Mwenyezi-Mungu zaenea hata mbinguni;uaminifu wako wafika mawinguni.
6. Uadilifu wako ni kama milima mikubwa,hukumu zako ni kama vilindi vya bahari.Wewe, ee Mwenyezi-Mungu, wawalinda wanadamu na wanyama