5. Utapanda tena mizabibujuu ya milima ya Samaria;wakulima watapanda mbeguna kuyafurahia mazao yake!
6. Maana siku yaja ambapo mlinzi atapiga mbiukatika vilima vya Efraimu:‘Amkeni, twende juu mpaka Siyonikwa Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu.’”
7. Maana Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Imbeni kwa furaha kwa ajili ya Yakobo,pigeni vigelegele kwa ajili ya taifa kuu,tangazeni, shangilieni na kusema:‘Mwenyezi-Mungu na awaokoe watu wake,amewaletea ukombozi waliobaki wa Israeli!’
8. Tazama, nitawaleta kutoka nchi ya kaskazini,nitawakusanya kutoka miisho ya dunia.Wote watakuwapo hapo;hata vipofu na vilema,wanawake waja wazito na wanaojifungua;umati mkubwa sana utarudi hapa.
9. Watarudi wakiwa wanatoa machozi,nitawarudisha nikiwafariji;nitawapitisha kando ya vijito vya maji,katika njia iliyonyoka ambamo hawatajikwaa;maana mimi nimekuwa baba wa Israeli,Efraimu ni mzaliwa wangu wa kwanza.
10. Enyi mataifa, sikilizeni neno langu mimi Mwenyezi-Mungu,litangazeni katika nchi za mbali,semeni: ‘Aliyemtawanya Israeli, atamkusanya,atamtunza kama mchungaji atunzavyo kondoo wake.’