15. Mwenyezi-Mungu amekuondolea hukumu iliyokukabili,amewageuzia mbali adui zako.Mwenyezi-Mungu, mfalme wa Israeli yuko pamoja nawehutaogopa tena maafa.
16. Siku hiyo, mji wa Yerusalemu utaambiwa:“Usiogope, ee Siyoni,usilegee mikono.
17. Mwenyezi-Mungu, Mungu wako yu pamoja naweyeye ni shujaa anayekuletea ushindi.Yeye atakufurahia kwa furaha kuu,kwa upendo wake atakujalia uhai mpya.Atakufurahia kwa wimbo wa sauti kubwa,
18. kama vile katika siku ya sikukuu.”Mwenyezi-Mungu asema:“Nitakuondolea maafa yako,nawe hutahitaji kuona aibu kwa ajili yake.