12. Ni chukizo kubwa wafalme kutenda uovu,maana msingi wa mamlaka yao ni haki.
13. Mfalme hupendelea mtu asemaye kwa unyofu;humpenda mtu asemaye ukweli.
14. Hasira ya mfalme ni kama mjumbe wa kifo;mtu mwenye busara ataituliza.
15. Uso wa mfalme ukingaa kuna uhai;wema wake ni kama wingu la masika.