9. Uchafu wake ulionekana waziwazi,lakini wenyewe haukujali mwisho wake.Anguko lake lilikuwa kubwa mno;hakuna awezaye kuufariji.Wasema:“Tazama ee Mwenyezi-Mungu mateso yangu,maana adui yangu ameshinda.”
10. Maadui wamenyosha mikono yao,wanyakue vitu vyake vyote vya thamani.Naam umeona watu wa mataifa wakiingia hekaluni,watu ambao Mwenyezi-Mungu aliwakatazakujumuika na jumuiya ya watu wake.
11. Watu wa Yerusalemu wote wanahangaika kutafuta chakula;hazina zao wanazitoa kupata chakula,wajirudishie nguvu zao.Nao mji unalia,“Hebu niangalie, ee Mwenyezi-Mungu,ona jinsi nilivyogeuka kuwa duni.
12. “Enyi wapita njia, hivi hamjali kitu?Tazameni! Hakuna aliyepatwa na uchungu kama mimi,uchungu alioniletea Mwenyezi-Mungu,siku ya hasira yake kali.
13. “Aliteremsha moto kutoka juu,ukanichoma hata mifupani mwangu.Alinitegea wavu akaninasa,kisha akanirudisha nyuma,akaniacha nimeduwaa na kuzirai mchana kutwa.
14. “Aliyahesabu makosa yangu yoteakayakusanya mahali pamoja;aliyafunga shingoni mwangu kama nira,nikafyonzwa nguvu zangu kwa uzito wake.Mwenyezi-Mungu aliniweka mikononi mwaowatu ambao siwezi kuwapinga.
15. “Mwenyezi-Mungu aliwakataa askari walionilinda,alitangaza wakati maalumu wa kuniadhibukuwaponda vijana wangu wa kiume.Aliwaponda kama katika shinikizowatu wangu wa Yuda.
16. “Kwa sababu ya hayo ninalia,machozi yanitiririka,sina mtu yeyote wa kunifariji;hakuna yeyote wa kunitia moyo.Watoto wangu wameachwa wakiwa,maana adui yangu amenishinda.
17. “Nainyosha mikono yangulakini hakuna wa kunifariji.Mwenyezi-Mungu ametoa amri dhidi yangu mimi Yakobo,jirani zangu wawe maadui zangu.Naam, mimi Yerusalemu nimekuwa kinyaa kwao.